Kakuma: Huduma za Habari- FilmAid Kenya (FAK)

FilmAid Kenya (FAK)

Sasisho la Mwisho: 18/1/2024

Maelezo

FilmAid hutoa taarifa kuhusu huduma zifuatazo: 

Msaada wa Kisheria

  • Maelezo kuhusu haki zako 

Huduma za Kijamii 

  • Maelezo kuhusu kuishi nchini Kenya 
  • Maelezo kuhusu Huduma za kijamii 
  • Maelezo kuhusu Mahali na jinsi ya kupata nyaraka ( kama nambari ya bima ya jamii, kibali cha kazi, leseni ya udereva, n.k.) 

Huduma za Afya 

  • Maelezo kuhusu Huduma za Afya na Mifumo ya Malalamiko, Maoni, na Msaada 

Huduma za WASH 

  • Taarifa kuhusu huduma za WASH  
  • Kuhamasisha usafi kupitia Mawasiliano ya Mabadiliko ya Kijamii na Tabia (SBCC) 

Shughuli za Kijamii za Burudani 

  • Mikutano za Maigizo na Sanaa  
  • Mikutano za Muziki 

Elimu 

  • Maelezo kuhusu jinsi ya kujiandikisha shuleni katika elimu ya msingi, sekondari, na programu ya elimu ya haraka 

Msaada wa Kipato/Ajira 

  • Maendeleo ya Ujuzi - Mafunzo ya Vyombo vya Habari (Upiga picha, Uandaaji Filamu) na Maigizo kwa Mabadiliko ya Kijamii  
  • Taarifa kuhusu kuanzisha biashara nchini Kenya  

Kurudi Nyumbani 

  • Maelezo kuhusu kurudi kwa hiari na msaada ulioandaliwa kurudi katika nchi yako ya asili 

Vigezo vya Kustahiki 

  • Huduma zote ni bure 

Upatikanaji 

  • Lugha zinazopatikana: Dinka, Kiarabu, Kisomali, Anyuak, Oromo, Kiswahili, Nuer, Dinka  
  • Mlango wa kuingilia eneo hili una paa la kupandia  
  • Eneo hili lina wafanyakazi wa kike 

Mahali/eneo 

Kakuma: FilmAid Kenya Offices, Kiwanja cha 3. 

Mifumo ya maoni ya taasisi  

  • Simu: +254722540834  
  • Muda wa kupokea maoni kutoka FilmAid - masaa 24 
  • Shirika litajibu kupitia simu na barua pepe  
  • Miadi inaweza kupangwa kupitia: +254722540834 

Anwani

Kakuma: FilmAid Kenya Offices, Compond 3.