Kakuma: Huduma za Taarifa-SIKIKA

SIKIKA

Kakuma: Huduma za Taarifa-SIKIKA logo

Maelezo

SIKIKA inatoa ukwaa la taarifa na mawasiliano Kakuma, Kalobeyei, na jamii inayowakaribisha wakimbizi katika eneo hilo. Vikundi vya Wasikilizaji 290 wanapokea programu ya sauti ya dakika 30-45 kila wiki ,ambayo inatengenezwa na wakimbizi na wenyeji.  

SIKIKA inashughulikia mada zifuatazo na nyinginezo: 

  • Afya 
  • Usafi wa Mazingira 
  • Ulinzi 
  • Elimu 
  • Michezo 
  • Hadithi za Mafanikio 
  • Mazingira/Hali ya Hewa/Mabadiliko ya Tabianchi 
  • Makazi 
  • Chakula/Lishe 
  • Kilimo 
  • Tangazo la Huduma za Umma 
  • Haki za Wakimbizi 
  • Usalama na Ulinzi  

Vigezo vya Kustahiki

  • Kila mkimbizi,mwanachama wa jamii ya wenyeji wanaweza kujiunga na Kikundi cha Kusikiliza SIKIKA

Jinsi Huduma Zako Zinavyopatikana Ili kuwa mwanachama wa Kikundi cha Kusikiliza

  • Tafadhali wasiliana na Kiongozi wa Kikundi cha Kusikiliza katika eneo lako.  

Eneo

  • SIKIKA ina Vikundi vya Wasikilizaji kote Kakuma, Kalobeyei, na maeneo ya jirani. Ofisi iko Kakuma, kiwanja cha 3.  

Mifumo ya Maoni ya Taasisi na Masaa ya Kazi

  • Baada ya kila kikao cha kusikiliza, vikundi hujadili programu na maudhui. Wanawasilisha maoni kwa chumba cha wahariri cha SIKIKA ambapo yanachambuliwa na kipindi kipya kinatengenezwa kulingana na maoni hayo.