Mnamo Novemba mwaka wa 2021, Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta alitia sahihi Sheria ya Wakimbizi ya 2021.

Sheria ya Wakimbizi ya 2021 inatambua ulinzi na usimamizi wa wakimbizi nchini Kenya. Sheria inatoa matumaini mapya kwa zaidi ya wakimbizi 500,000 kwani sasa watapata riziki na ushirikiano wa kiuchumi na kijamii.

Kenya ilianza kutumia sheria hii mpya ya wakimbizi mnamo Februari 23, 2022.

Makala haya yanaangazia mambo muhimu ambayo unahitaji kujua kuhusu Sheria ya Wakimbizi ya 2021. Pitia nakala hii kwa utaratibu ili kuelewa mabadiliko, haki mpya na fursa zinazoweza kuathiri maisha ya wakimbizi, wanaotafuta hifadhi nchini Kenya.

SWA_Refugee_Act_2021.png

Kwanza, Sheria ya Wakimbizi ya 2021 inatanguliza idadi ya haki kwa wakimbizi na wanaotafuta hifadhi nchini Kenya. Haki mpya ni pamoja na;

  • Kushiriki katika maendeleo ya kiuchumi na kijamii mara tu wanapopokea hati na vibali vinavyofaa kutoka kwa serikali ya kaunti na ya kitaifa. Hii ina maana kwamba, wakimbizi sasa wanaweza kuwa katika ajira yenye faida na watatarajiwa kulipa kodi kama vile raia wa Kenya.
  • Wakimbizi wana haki ya kujihusisha na ajira au kuanzisha biashara au kufanya biashara katika sekta ambazo walizohitimu na zinazotambuliwa na mamlaka husika.
  • Haki ya kupata kitambulisho na hati za usajili wa raia kwa madhumuni ya kupata haki na huduma chini ya Sheria ya Wakimbizi ya 2021.
  • Wakimbizi kutoka mataifa ya Burundi, Rwanda, Sudan Kusini, Tanzania, Uganda wako na fursa ya kubadili hali yao ya kuwa wakimbizi na kutafuta uraia katika mataifa hayo chini ya taratibu na itifaki za Muungano wa Kiuchumi wa Jumuia ya Afrika ya Mashariki maarufu kama (EAC).
  • Kujumuishwa kwa wakimbizi katika mipango ya maendeleo ya kitaifa na kaunti ikijumuisha matumizi ya pamoja ya taasisi za umma, vifaa na nafasi kati ya wakimbizi na jamii zinazowapokea.
  • Ulinzi wa wakimbizi na wanaotafuta hifadhi dhidi ya kurejeshwa kwa nguvu katika nchi zao za asili (kurejeshwa) isipokuwa pale ambapo kuna sababu zinazoeleweka kwamba wanachukuliwa kuwa hatari kwa usalama wa taifa la Kenya.
  • Kuongezwa kwa muda wa kukata rufaa kwa ombi la hadhi ya mkimbizi iliyokataliwa kutoka siku 30 zilizopita hadi siku zisizozidi 60.

Chini ya sheria mpya, mtu atahitimu kuwa mkimbizi nchini Kenya ikiwa:

  • Wamethibitisha kuwa na uoga kutokana na  kuteswa kwa misingi ya rangi, dini, utaifa, uanachama wao katika kundi fulani la kijamii au maoni ya kisiasa, na ikiwa watu hao hawataki kujitolea kwa ajili ya ulinzi wa nchi yao.

REFUGEE_ACT_2021_swa2.png

Makosa ya adhabu kwa wakenya, wakimbizi na wanaotafuta hifadhi nchini Kenya

Sheria ya Wakimbizi ya 2021 imeorodhesha matukio yoyote ya usajili mara mbili kama kosa la jinai na adhabu zinazojumuisha kifungo. Ni kosa la jinai kwa;

  • Raia yeyote wa Kenya kutuma maombi au kusaidia Mkenya mwingine kwa kujua katika ombi la kusajiliwa kama mtafuta hifadhi au mkimbizi.
  • Mkimbizi yeyote kutuma maombi ya Kitambulisho cha Kitaifa cha Kenya au pasipoti makusudi au kumsaidia mkimbizi mwingine au mtafuta hifadhi kutuma ombi hili.

Chini ya Sheria, ikiwa atapatikana kuwajibika, mtu huyo atalipa faini isiyozidi elfu 500 au kufungwa kwa muda usiozidi miaka mitatu au vyote kwa pamoja. Kutoa taarifa za uongo kwa afisa aliyeteuliwa kwa madhumuni ya kupata au kusaidia mtu mwingine kupata kibali, na au kujiandikisha kama mtafuta hifadhi au mkimbizi pia huorodheshwa kama kosa.

Ni hatia kwa mkimbizi, kuingia katika ndoa kwa lengo la kumsaidia mkimbizi mwingine kupata manufaa yoyote anayopewa na Sheria ya Wakimbizi ya 2021.

Ikiwa unaomba hifadhi nchini Kenya na huripoti kwa afisa aliyeidhinishwa ili kuomba hifadhi au kutambuliwa kama mkimbizi ndani ya siku 30 baada ya kuingia nchini Kenya uko katika hatari ya kuadhibiwa pia, ni kosa. Adhabu kwa yeyote atakayepatikana na hatia kwa hili ni pamoja na kuwajibika kulipa faini isiyozidi Kshs.50,000 au kifungo cha muda usiozidi miezi 6 au vyote kwa pamoja. Faini hiyo imeongezwa kutoka Kshs.20,000.

Pia ni kosa la jinai chini ya Sheria hii kuwa mkimbizi anayefanya kazi yenye faida nchini Kenya bila malipo ya kodi.

Vitendo vingine vilivyoorodheshwa kuwa makosa katika Sheria hiyo ni;

  • Kughushi, kubadilisha, kuharibu au kuharibu kwa makusudi kitambulisho au hati nyingine yoyote iliyotolewa chini ya Sheria ya Wakimbizi ya 2021.
  • Kuomba rushwa kutoka kwa mkimbizi/mtafuta hifadhi ili kurahisisha upatikanaji wa huduma au haki zao.

Julisha.Info imetoa majibu kwa baadhi ya maswali ambayo unaweza kuwa nayo kuhusiana na sheria mpya. Unaweza kupata majibu hapa.

 

Ikiwa una maswali yoyote kuhusu Sheria ya Wakimbizi ya 2021, tafadhali tuandikie kupitia ukurasa wetu wa Facebook Julisha.Info, Jumatatu hadi Ijumaa kuanzia 08:00 a.m. hadi 5:00 p.m.